WITO
umetolewa kwa jamii kuacha tabia ya
kufanya shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji ama maeneo kuzunguka
Milima ya Uluguru ili kuepusha na
uharibifu wa mazingira.
Wito huo
umetolewa jana na Mwenyekiti wa Shirika linalojihusisha na uhifadhi wa mazingira na uhamasishaji Mkoani Morogoro ‘’Tanzania environmental
and suntation concervetors (TESCO)
Ndumey Mukama wakati akizungumza na Mtanzania ofisini kwake.
Mukama amesema
kuwa
uharibifu wa mazingira umekuwa ukifanyika katika vyanzo vya maji na
maeneo yanayozunguka milima ya Uluguru na hiyo inatokana na jamii kutokuwa na
elimu ya kutosha kuhusu umuhimu wa utuzaji wa mazingira.
Aklitolea
mfano wananchi wamekuwa wakivuka mipaka
ya milima ya Uluguru na kufanya shughuli za kibinadamu na hivyo kuharibu
uoto wa asili.
Amesema kuwa bado
kuna changamoto ya utiririshaji wa maji machafu katika mabomba na pia katika mito ambayo
wananchi wanatumia maji hayo katika shughuli mbalimbali.
.
Aidha amesema
kuwa ili kukabiliana na changamoto hizo
za uharibifu wa mazingira Shirika limekuwa likitoa elimu ya mazingira mara kwa
mara ili kuwajengea wananchi uelewana kuona umuhimu wa utunzani mazingira yanayowazunguka.
Hata hivyo
amesema kuwa wamejaribu kutoa elimu ya mazingira ili wananchi waache
tabia ya kuchoma mioto katika safu za milima ya Uluguru lakini bado vitendo hivyo vya uharibifu wa
mazingira vinaendelea.
Post a Comment