BREAKING NEWS

Sunday, 7 February 2016

Ummy Mwalimu amekuwa mgeni rasmi katika siku ya kupinga ukeketaji duniani, kitaifa mkoani Dodoma

image1


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu leo amekuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Kupinga Ukeketaji Duniani yanayofanyika tarehe 5 Februari kila mwaka. Maadhimisho hayo kwa Mkoa wa Dodoma yalifanyika katika Ukumbi wa Hazina Dodoma, kwa kuratibiwa na Mtandao wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanayopinga Ukeketaji Tanzania.
Wakati wa maadhimisho hayo Mhe Waziri Ummy Mwalimu alieleza kuwa Kwa mujibu wa Takwimu za Demografia na Afya Tanzania (Tanzania Demographic and Health Survey – TDHS 2010) asilimia 15  ya wanawake Tanzania wamefanyiwa Ukeketaji. Ukeketaji ni ukatili dhidi ya watoto wa kike na wanawake. Na ni kosa la jinai. Madhara ya ukeketaji ni pamoja na vifo, vilema na maradhi kama fistula na mengineyo.
Alieleza kuwa Serikali itaendelea kukemea na kupambana na vitendo hivi katika jamii zetu. Na itaongeza jitihada za kutoa elimu kwa jamii sambamba na kuwachukulia hatua wote wanaojihusisha na vitendo hivi.
Mhe Waziri Ummy Mwalimu aliwataka Maafisa Maendeleo ya Jamii katika Mikoa.
Wilaya na Kata kuongeza nguvu ktk kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa lengo la kuhakikisha wazazi/walezi, mangariba na wote wanaojihusisha na vitendo vya Ukeketaji wanafikishwa ktk vyombo vya dola ili sheria ichukue mkondo wake.
Aidha, alitoa wito kwa kila mwananchi kushiriki katika mapambano haya hasa katika kutoa taarifa na ushahidi Mahakamani.
image4 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akipokea maandamano ya wadau mbalimbali wa Maendeleo ya Mtoto katika viwanja vya ofisi za Hazina Dodoma wakati wa maadhimisho ya Siku ya kupinga ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike.
image2 
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akihutubia wadau mbalimbali wa Maendeleo ya Mtoto, wakati wa maadhimisho ya Siku ya kupinga ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike

image8 

image7image1Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (mstari wa mbele katikati), Mkuu wa wilaya ya Dodoma  Dkt. Jasmine Tisekwa ( Kulia) na Muwakilishi wa UNFPA, Bi Christine Mwanukuzi ( Kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa Mtandao wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanayopinga Ukeketaji Tanzania, wakati wa maadhimisho ya Siku ya kupinga ukeketaji kwa wanawake na watoto wa kike.  

Share this:

 
Back To Top
Distributed By Rodrick Minja | Designed By Bill De Pierree