BREAKING NEWS

Monday, 8 February 2016

Waziri Simbachawene Apongeza Uchaguzi wa Meya Dar es Salaam Kuahirishwa



 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene amesema Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, imetumia busara kuahirisha uchaguzi wa Meya uliopangwa kufanyika leo.

Juzi halmashauri hiyo, iliahirisha uchaguzi huo, ikiwa ni mara ya pili baada ya kubaini nyongeza ya wajumbe 14 katika orodha iliyowasilishwa kwa wakurugenzi wa Manispaa za Kinondoni na Ilala.

Kasoro hizo zilijitokeza katika kikao cha viongozi wa halmashauri hiyo kilichongozwa na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Sarah Yohana na kuhudhuriwa na viongozi wa CCM, Chadema na CUF kujadili ajenda mbili.

Ajenda hizo ni taratibu za kuendesha uchaguzi wa Meya na kupitia orodha ya wajumbe wanaostahili kushiriki.

Kutokana na hali hiyo, ilimlazimu Yohana kuwaagiza wakurugenzi wa manispaa za Kinondoni na Ilala kuyafanyia uhakiki majina hayo wakishirikiana na viongozi wa vyama ili kuyapeleka halmashauri kesho kutwa.

Simbachawene alisema jana kuwa halmashauri na viongozi wa vyama hivyo walitafakari maelezo aliyoyatoa awali kabla kufikia hatua ya uchaguzi huo.

“Sijapata taarifa za kuahirishwa ndiyo kwanza nasikia kwako, lakini kama sababu ndiyo uliyoniambia basi wamefanya jambo jema. Kwa sababu uchaguzi huu una mvutano hivyo ni lazima mambo yaende kwa makubaliano.

“Pia ni hatua nzuri, itakayoleta maelewano baina yao ili kupata haki sawa kwa wajumbe watakaostahili kupiga kura. Tamisemi kazi yetu ni kueleza sheria inasemaje,” Simbachawene.

Hivi karibuni, Simbachawene aliahirisha uchaguzi huo, kisha kutoa sababu kuwa ni kuandaa mfumo wa upatikanaji wa wajumbe kutoka manispaa tatu kwa kuwa ule wa chama kimoja haukuwa na shida kama ilivyo sasa.

Katibu wa Chadema, Kanda ya Dar es Salaam, Henry Kilewo alisema kukwama kwa uchaguzi huo kunatokana na viongozi kutosikiliza mawazo ya upinzani.
 “Januari 27, nilimwandikia barua Simbachawene ya kutaka atupatie utaratibu wa uchaguzi huu utakavyokuwa, lakini hadi leo (jana), hakunijibu ndiyo maana matatizo kama haya yanatokea,” alisema.

Share this:

 
Back To Top
Distributed By Rodrick Minja | Designed By Bill De Pierree